Social Icons

NIFA AD

NIFA AD

NIFAAAA

NIFAAAA

Wednesday, August 11, 2021

MSUMARI WA MWISHO WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUHUSU SAKATA LA TOZO ZA SIMU:


 Rais Samia Apigilia Msumari wa Mwisho Sakata la Tozo Kwenye Simu

Rais wa awamu ya sita wa Tanzania Samia Suluhu Hassani amesema serikali inawashukuru wananchi kwa kukubari kuchangishana kwa ajili ya tozo kwenye miamala ya simu.

Rais Samia amesema wananchi wamekuwa wakilalamila juu ya kiwango cha makato na sio tozo kam watu wengi wanavyoripoti na serikali imeleta sera hiyo ili kusaidia.

“Lalamiko kubwa la wananchi ilikuwa kiasi cha makato kinachoweka kwenye tozo wamekubari kuchanga na nashukuru kwenye hilo, maan tunataka tujenge vituo vya afya vingi, tunawabana wananchi kwa faida yao kila mtu ametoka kwenye hali ngumu hivyo tukichangishana inakuwa kwa faida yao”

Hii inakuwa ni mara ya pili kwa Rais Samia kusisitiza kuwa tozo hizo zinafaida kubwa kwa wananchi licha ya malalamiko kadhaa ya wananchi kuhusu tozo hizo

Je umezikubali tozo kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu? Toa maoni yako hapa.

0 comments:

Post a Comment

 
 
Blogger Templates