Monday, July 26, 2021
WIZARA YA AFYA IMETOA TAHADHARI YA MIKUSANYIKO.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kpitia katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Abel Makubi, Jana Julai 25, 2021 ametangaza hatua ya kupiga marufuku kwa mikusanyiko isiyo ya lazima ikiwemo mikusanyiko ya kidini na ya kisiasa ambayo itaendelea hadi janga hilo litakapodhibitiwa.Pia amesisitiza kuimarisha hatua za tahadhari kwenye migahawa, mikutano, sherehe za harusi na mazishi. Ametaka kuwekwa vipima joto, vifaa vya kunawia mikono kwenye sehemu za umma, watu kuvaa barakoa na kudumisha umbali mzuri wa kijamii.
Tanzania imepokea dozi zaidi ya milioni moja za chanjo ya virusi vya Corona kupitia mpango wa COVAX.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 comments:
Post a Comment