Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya Teknolojia habari na Mawasiliano imetoa muongozo juu ya tozo ya laini za simu kiasi cha Sh10 hadi Sh200 kulingana na uwezo wa kuongeza salio wa mtumiaji na Makato ya tozo hizo yamemepanga kuanza Agosti 1 mwaka huu.
Tufahamu kwa kipindi wananchi wapo katika kipindi cha kutoa maoni baada ya makato kwenye miamala kupanda, wakiwa bado hawaja shusha pumzi vizuri wanakutana na tozo ya salio kwenye laini zao za simu.
Uzalendo kwa kulipa kodi ni jukumu kwa kila mtanzania inabidi kila mwananchi achangie kwa njia yoyote kulipa kodi ili kuimarisha uchumi wa Taifa.

0 comments:
Post a Comment