Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema makampuni ya mitandao ya Kijamii yatatozwa faini ya asilimia 10 toka kwenye mapato yao kama wakishindwa kuondoa vitendo na maneno ya kibaguzi kwenye mitandao yao.
Boris Johnson ameyasema hayo leo Bungeni kufuatia baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya England kutolewa maneno ya kibaguzi baada ya kushindwa kuchukua ubingwa wa EURO 2020 siku ya Jumapili. Aidha amesema kwa mtu yeyote ambaye atakutwa na hatia, basi atafungiwa maisha kuingia kwenye uwanja wowote wa mchezo wa mpira wa miguu.

0 comments:
Post a Comment