Raia wa Nigeria wataona vichwa vya habari vinavyofanana katika magazeti yote nchini humo kwa siku ya Jumatatu Julai 12 na Julai 13.
Hii ikiwa ni kampeni ya tasnia ya habari iliyoanzishwa na wahariri, waandishi na wamiliki kupinga kutangazwa kwa miswada itakayodhoofisha uhuru wa vyombo vya habari nchini humo.
Taarifa hiyo ikiwa na neno la 'taarifa kufungiwa' na picha inayomuonesha mtoto akiwa katika nguzo za gerezani zinazomfunga mdomo.
Baraza la habari nchini Nigeria (NPC), na tume ya utangazaji ya taifa (NBC) imetoa orodha ya mswada ambao utamtaka mwandishi au mmiliki wa chombo cha habari kulipishwa faini ya dola $12,100 kwa kutoa habari isiyo na ukweli na kutokuwa huduma isiyokuwa na viwango bora.
Kama mswada huo utapitishwa na kuwa sheria, wale watakao kamatwa watafungwa gerezani kwa kipindi cha miaka mitatu.
Mwezi uliopita mwenyekiti wa Jumuiya ya kitaifa wa seneta ya tume ya vyombo vya habari na utangazaji, seneta Ajibola Basiru, alitetea mswada huo.
"Ukweli ni kwamba mtu anayesimamia shughuli za vyombo vya habari kama redio, televisheni haimaanishi kuwa anataka kuminya uhuru wa vyombo vya habari, "alisema.
Jumuiya ya waandishi wa habari (NUJ), Chama cha wahariri Nigeria (NGE) na Jumuiya ya wamiliki wa magazeti (NPAN) wanaamini kuwa sababu ya marekebisho ya sheria hiyo ni kutaka kuwa na uwezo wa kudhibiti na kufuatilia kile watakachokichapisha, " ambapo pia inawanyima jamii haki ya kusikilizwa au kusikia kile kilicho haki yao’", walisema.
Kampeni hii itadumu kwa muda wa siku mbili.

0 comments:
Post a Comment