Jeshi la China limesema "limeifukuza" meli ya kivita ya Marekani ambayo lilisema iliingia kinyume cha sheria katika Eneo la bahari ya China karibu na Visiwa vya Paracel vyenye mgogoro Jumatatu, wakati wa kumbukumbu ya uamuzi wa kihistoria wa mahakama ya kimataifa kwamba Beijing haina madai juu ya Bahari ya Kusini mwa China.
USS Benfold iliingia kwenye maji ya Paracels bila idhini ya serikali ya China, ikikiuka sana uhuru wa China na kutishia hali ya utulivu wa Bahari ya Kusini mwa China, Kikosi cha Kusini mwa Jeshi la Wananchi kilisema.
"Tunaihimiza Marekani kuacha mara moja vitendo vya uchokozi," Kitengo hicho cha jeshi kimesema kupitia taarifa
Katika taarifa, Kikosi cha 7 cha Jeshi la Wanamaji la Marekani kimesema Benfold "Imeshikilia haki na uhuru wa kusafiri karibu na Visiwa vya Paracel, kwa mujibu wa sheria za kimataifa" na ikatupilia mbali madai ya Wachina ya ukiukaji mkubwa wa kuingia katika eneo lake kama "ya uwongo" na upotoshaji.

0 comments:
Post a Comment