Wimbo wa @wizkidayo "Essence" ft. @temsbaby umeingia katika chart kubwa duniani za Billboard Hot 100
Ngoma hiyo imefanikiwa kuingia katika chart hizo na kukamata nafasi ya 82 ikiwa ni baada tu ya mkwaju huo kuuza nakala 40,000 nchini Marekani wiki iliyopitwa
Hii inakuwa mara ya tatu kwa mkali huyo wa Nigeria kuingia kwenye chart hizo, kwani kwa mara ya kwanza aliingia hadi namba 1 kupitia "One Dance" wimbo ambao alipewa shavu na Drake mwaka 2016, wimbo huo ulikaa namba 1 kwa wiki 10. Mara ya pili aliingia kupitia wimbo wa "Brown Skin Girl" alioshirikishwa na Beyonce.
Pia hii inakuwa ndio ngoma ya kwanza ya kutoka Nigeria kuingia katika Chart hizo kubwa duniani ambayo inamilikiwa na star huyo.
Vile vile #Tems anakuwa mara yake ya kwanza kuingia kwenye charts hizo za #BillboardHot100
Unadhani ni Star gani hapa nchini ataingia kwenye Chart hizo kubwa duniani ?

0 comments:
Post a Comment