Friday, October 22, 2021
DIAMOND KUWANIA TUZO ZA MTV EUROPE MUSIC AWARDS.
Nyota muziki wa Bongoflava na Tanzania, Diamond Platnumz @diamondplatnumz amechaguliwa kuwania tuzo za MTV Europe Music Awards (MTV EMA) 2021.
•
‘Simba’ atachuana na wasanii wengine wanne kutoka Afrika, Tems (Nigeria), Wizkid (Nigeria), Focalistic (Afrika Kusini) na Amaarae (Ghana) kuwania taji la mwaka huu la Best African Act.
•
Katika hatua itakayowaacha wapenzi wa muziki wa kiafrika vinywa wazi, Nyota mwingine wa Afrika ambaye pia ni mshindi wa Grammy, Burna Boy hakutajwa katika kitengo chochote.
•
Washindi watatuzwa katika hafla itakayoandaliwa Papp László Budapest Sportaréna jijini Budapest, Hungary, November 14 .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment