Tuesday, September 7, 2021
MADEE NA JANJARO WAGUSWA NA MTOTO WILSON.
Wasanii Madee Ally na Dogo Janja wamefunga safari mpaka nyumbani kwa mtoto Wilson, Yombo Kwa Limboa baada ya kuguswa na habari yake walioiona kupitia makala ya Shabaha ya @Cloudstv.
Mtoto huyo WILSON amekuwa akiishi bila vidole vya mikono na miguu kwa muda wa miaka minne sasa yaani tangu kuzaliwa kwake.
Tatizo hilo limepelekea ashindwe kutembea vizuri na kutoweza kushika chochote mkononi ambapo anahitaji kufanyiwa upasuaji ili aweze kuwa sawa.
Unaweza kuendelea kuungana na kina Madee kumsaidia Wilson ili aweze kukamilisha fedha za matibabu kupitia namba 0692 572068 JINA ROBERT JOHN
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment