Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetoa tamko juu ya ile vuta ni kuvute ya Kamati ya Miss Tanzania pamoja na Miss Tanzania 2020/21 Rose Manfere.Iliripotiwa kuwa Manfere alikiuka baadhi ya masharti ya mkataba wake. Hivyo kamati hiyo ikatangaza Manfere hataweza kushiriki mashindano ya urembo wa dunia yanayotarajiwa kufanyika Desemba 2021 nchini Puerto Rico na badala yake aliyekuwa mshindi namba mbili, Juliana Rugimisa ataliwakilisha Taifa.
Basata limetangaza kuwa halijaridhia na halikubaliani na maamuzi ya Kamati ya Miss Tanzania bila kutoa sababu za msingi.

0 comments:
Post a Comment