Social Icons

NIFA AD

NIFA AD

NIFAAAA

NIFAAAA

Sunday, July 11, 2021

MICHELLE; NASHUKURU MUME MWENYE NDOTO ZANGU.

 


Wengi kati yenu mnapenda kumuita Michelle Obama siyo kama mnakosea hapana lakini haya ndio majina aliyopewa baada tu ya kuzaliwa na kuuona uso wa dunia, jina la kuzaliwa ni Michelle LaVaughn Robinson), amezaliwa mnamo tar. 17 Januari 1964) ni Mwanasheria wa Kimarekani na ndiyo mke wa Rais mstaafu wa awamu ya 44 wa Marekani Bw. Barack Obama. Huyu ndiye Mwafrika Mwamerika wakwanza kuwa Mwanamke wa Kwanza wa Marekani.

Michelle alizaliwa na kukulia katika kitongoji cha South Side ya Chicago na kusoma hadi kuelekea katika Chuo Kikuu cha Princeton halafu baadaye katika Kitivo cha Sheria cha Harvard.

Baada ya kumaliza elimu yake hiyo, alirudi Chicago na kukubali kuchukua nafasi ya kazi katika kampuni ya Sidley Austin, halafu baadaye akaja kuwa kama mmoja kati ya wafanyakazi wa meya wa Chicago Bw. Richard M. Daley, halafu baadaye akafanya kazi katika Chuo Kikuu cha Chicago na Hospitali za Chuo Kikuu cha Chicago.

Michelle Obama ni dada wa Craig Robinson, kocha wa mpira wa kikapu wa Oregon State University. Alikutana na Barack pale alipojiunga na Sidley Austin. Pale Barack Obama alipochaguliwa kuwa kama Seneta, familia ya Obama ikachagua kuishi mjini Chicago South Side kuliko kuishi mjini .Washington D.C.Kati ya ndoto kubwa ya Michelle alitamani sana kuja kuolewa na mwanaume mwenye ndoto za kuja kuwa Raisi wa marekani, kwa kuwa mungu hamtupi mja wake ndoto hiyo ya Michelle ilitimia mwaka 2008 baada ya Obama kutangazwa ndio Raisi wa 44 kupitia chama cha Democratic.

             Mwandishi; F.A.Maige.

          Usisahau kupita kwenye blog yetu pendwa kila siku kusoma habari na matukio ya siasa na burudani kwa maoni na ushauri weka maoni yako.Asante

 

 

0 comments:

Post a Comment

 
 
Blogger Templates