Social Icons

NIFA AD

NIFA AD

NIFAAAA

NIFAAAA

Saturday, July 17, 2021

RAIA WA SOMALIA APIGWA RISASI NA KUUAWA KWA KOSA LA KUMBAKA MWANAE WA KAMBO.

 


Mwanaume mmoja nchini Somalia ameuawa kwa kupigwa risasi kusini mwa nchi hiyo na serikali ya Jimbo la Jubaland baada ya kumbaka binti yake wa kambo mwenye umri wa miaka mitatu ambaye alifariki kutokana na majeraha ya kubakwa.

Mahakama katika mji wa Dhobley imemkuta Hussein Adan Ali mwenye umri wa miaka 28 na hatia siku ya Jumatano, kama ilivyotangazwa katika kituo cha Televisheni cha eneo hilo.

Viongozi wa jadi na maofisa wa mahakama walipitia ushahidi kabla ya kutekeleza hukumu hiyo.

Kwa mujibu wa ushahidi uliowasilishwa, Ali alikuwa amekula mirungi wakati alipomfanyia unyanyasaji huo mtoto wake.

Haijaweka wazi tukio hilo lilitokea wapi lakini mahakimu wamesema mtoto amefariki Jumatano.

Matangazo ya Televisheni hayakuonesha kama mawakili walihudhuria mahakamani au mshutumiwa kama alipata fursa ya kukata rufaa.

Hukumu hiyo ya kifo ilitolewa chini ya sheria za kiislamu, mahakama ilisema.

Televisheni ya taifa ya Somalia iliweka picha ya Ali katika kurasa yake ya twitter:

Social embed from twitter


0 comments:

Post a Comment

 
 
Blogger Templates