Kim Jong-un (matamshi ya Kikorea:
[kim.dzʌŋ.ɯn] au [kim.tsʌŋ.ɯn]; alizaliwa 8 Januari 1982-1984 au 5 Julai 1984)
ni Mwenyekiti wa Chama cha
Wafanyakazi wa Korea (WPK) na kiongozi mkuu wa Korea ya Kaskazini.
Kim ni mtoto wa pili wa Kim Jong-il (1941-2011)
na Ko Yong-hui. Kabla ya kuchukua madaraka, Kim alikuwa haonekani mara kwa mara
kwa umma. Maelezo kama vile mwaka gani alizaliwa, na kama alienda kweli shule
nchini Uswisi akitumia
jina la uongo, ni vigumu kuthibitisha.
Tangu mwaka 2009 taarifa zilianza kutokea kuwa Kim
aliteuliwa kumfuata baba yake aliyekuwa mgonjwa, akipewa nafasi katika kamati
ya kijeshi[1].
Nyimbo zilianza kutungwa za kusifu familia ya Kim zikitaja jina la Kim Jong-Un.[2] Mwaka
2010 alipewa cheo cha jenerali jeshini na kuwa makamu wa mwenyekiti wa kamati
kuu ya kusimamia jeshi[3].
Kim alitangazwa kuwa kiongozi mkuu baada ya mazishi ya
baba yake tarehe 28 Desemba 2011. Vyeo vyake ni Mwenyekiti wa Chama cha
Wafanyakazi wa Korea, Mwenyekiti wa Tume Kuu ya Kijeshi, Mwenyekiti wa Tume ya
Mambo ya Ndani, Kamanda Mkuu wa Jeshi la Watu wa Korea, na mwanachama wa Kamati
ya Kudumu ya Politburo ya Chama cha Wafanyakazi wa Korea. Mamo tarehe 9 Machi
2014, Kim Jong-un alichaguliwa bila kupingwa kuingia katika Bunge Kuu la Watu.
Kim ana shahada mbili, moja ya fizikia kutoka Chuo Kikuu cha Kim Il-sung,
na nyigine kama afisa wa Jeshi katika Chuo Kikuu cha Jeshi cha Kim Il-sung.
Tarehe 12 Desemba 2013, vyombo vya habari vya Korea
Kaskazini vilitangaza kwamba kwa sababu ya "udanganyifu," aliamuru
mauaji ya mjomba wake Jang Song-thaek. Kim
Jong-un anaaminika kuwa ndiye aliyeamuru mauaji ya kaka yake wa kambo, Kim Jong-nam nchini
Malaysia mwezi Februari 2017.Mara zote duniani kuna kuwa na utaratibu wa
kufanya uchaguzi kwa viongozi wa nchi ikiwemo Raisi na wabunge ni kila baada ya
miaka 4 au 5 lakini kwa Korea kaskazini ni tofauti kidogo kila inapofika wakati
wa uchaguzi kaika nchi hyo bhasi ni ruhusa kwa Kim jung _un yeye pekee ndio anayepata
ruhusa ya kupiga kura.
Mwandishi;
F.A.Maige.
Simu no.0657
129 225.
Usipitwe na
ukarasa huu kila wakati.
0 comments:
Post a Comment